- 7,623 viewsDuration: 3:11Rais William Ruto ameendeleza shutuma zake dhidi ya Rais Mstaafu Uhuru Kenyatta, akidai kuwa anawatuma viongozi wa upinzani kuhujumu miradi ya maendeleo ya serikali. Akizungumza katika Kaunti ya Migori, Ruto aliwataka Wakenya kupuuza kile alichokitaja kuwa ni hadaa za upinzani, akisema viongozi hao hawana mpango wala tajriba ya kuendeleza taifa kwa manufaa ya vizazi vijavyo.