- 41 viewsKamati ya bunge la kitaifa kuhusu kawi na Petroli sasa ilidai majibu kwa serikali kuhusu shehena ya mafuta iliyozua utata huku ikisema haikuridhishwa na maelezo ya waziri Opiyo Wandayi kuhusu sakata hiyo. Kamati hiyo inayoongozwa na mbunge wa nakuru town east David Gikaria ilifanya ziara katika kampuni ya Kenya Pipeline kutathmini kiwango cha mafuta ambapo ilibaini kuwa hakuna uhaba wa petroli. Kamati hiyo ikitaka leseni za wafanyabiashara walioficha mafuta kubatilishwa