- 123 viewsDuration: 1:19Serikali inatoa hamasisho kwa wazazi kuwasajili wana wao walio na ulemavu wa aina yoyote ili kupata elimu. Akizungumza katika hafla ya michezo ya watoto walio na ulemavu kaunti ya Kisumu, katibu katika idara ya watoto Carren Angeng’o alisema kuwa takwimu za serikali zinaonyesha kuwa ni watoto milioni moja nukta mbili pekee waliosajiliwa, huku idadi kubwa ikikumbwa na unyanyapaa.