- 1,489 viewsDuration: 2:24Viongozi wa kiislamu kutoka kaunti ya kitui wamelaumu shule ya upili ya st. Ursula Tungutu kwa kuwanyima nafasi wasichana wa dini la kiislamu kuvaa hijabu shuleni Viongozi hao wamekashifu kitendo hicho wakitaka wizara ya elimu kuingilia kati, wakisema kuwa wanafunzi watano walilazimishwa kutoa hijabu na kuadhibiwa shuleni. Wamedai kuwa katiba ya Kenya imeruhusu mavanzi ya kuheshimu dini ilhali kuna baadhi ya shule zinazokiuka sheria hiyo. Juhudi zetu za kuzungumza na mwalimu mkuu wa shule hiyo Jackline Kusunza hazikufua dafu kwani mlinda lango aliwazuia wanahabari kuingia shule humo.