Tume ya kupambana na ufisadi nchini ilivamia ofisi za serikali ya Kaunti ya Embu kuhusiana na madai ya kashfa ya kandarasi ya thamani ya Shilingi milioni 95 inayowahusisha wawakilishi wadi watatu na maafisa wa serikali ya kaunti hiyo.
Wapelelezi waliwavamia nyumba nane na kupiga kambi katika makao makuu ya kaunti, wakichukua nyaraka za ununuzi, maelezo ya malipo, na faili za kandarasi. wawakilishi wadi hao wanashukiwa kuwa na nia ya kufaidika katika kampuni angalau kumi na moja zilizopewa kandarasi kinyume cha sheria.