Huku makataa ya kuwasilisha kesi za waathiriwa wa maandamano ambayo ni tarehe tatu aprili yakikaribia, mwenyekiti wa tume ya kutetea haki za binadamu claris ogangah, ametoa wito kwa waathiriwa kujitokeza katika ofisi za tume hiyo au kupitia njia za kidijitali ili kuorodheshwa kwenye mpango wa kitaifa wa fidia ..waathiriwa na familia zilizopoteza wapendwa wao wanatakiwa kuwasilisha stakabadhi muhimu kama fomu za p3 na ripoti za matibabu ili kuhakikisha haki inatendeka kupitia mfumo wa fidia na marekebisho.