- 985 viewsDuration: 1:09Upasuaji wa maiti umethibitisha kuwa watu wawili waliouawa wakati wa maandamano eneo la ishiara kaunti ya Embu walifariki kwa kuvuja damu kufuatia majeraha ya risasi. Uchunguzi wa maiti uliofanyika hospitali ya rufaa ya kaunti ya embu leo na kuongozwa na mpasuaji wa maiti wa serikali dkt. Grace midigo, ulionyesha kuwa mmoja alipata jeraha la risasi shingoni huku wa pili alisalia na risasi iliyopitia mdomoni. Risasi hiyo ilitolewa na kukabidhiwa maafisa wa upelelezi .