- 3,486 viewsDuration: 3:05Kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa, uhaba wa maziwa umeendelea kushuhudiwa nchini, huku serikali ikikosa suluhu mwafaka ya kukabiliana na hali hiyo. Uhaba huo sasa umechangia kupanda kwa bei ya maziwa, huku maduka makuu yakiweka kikomo cha kiwango cha maziwa ambacho kila mteja anaruhusiwa kununua. Hali hii imeibua lawama kutoka kwa wakulima, wanaoilaumu serikali kwa kuchangia kuongezeka kwa bei ya chakula cha mifugo.