- 28 viewsDuration: 2:14Huku mvua ikiendelea kushuhudiwa katika sehemu mbali mbali humu nchini, wakaazi wa eneo la Mikiryani eneo bunge la Kaloleni kaunti ya Kilifi wanaomba wahisani kuingilia kati na kurekebisha mapaa ya shule ya msingi ya Mikiryani kwa hofu ya uharibifu kutokana na upepo mkali unaoambatana na mvua. Wakizungumza na wanahabari baada ya kupokea mabati na mbao za kurekebisha baadhi ya madarasa kutoka kwa shirika la Gapeka Children Hope Center wakaazi hao wamesema kuwa zaidi ya madarasa kumi katika shule hiyo yanavuja hali ambayo inatatiza masomo kwa wanafunzi kando na kuwepo hatari ya kuangukiwa na mapaa hayo.