- 290 viewsDuration: 1:10Baadhi ya viongozi wa kisiasa katika kaunti ya Nyamira wamewashauri vijana kujitokeza kwa wingi na kujisajili kuwa wapigakura kwenye zoezi linaloendelea kote nchini. Wakizungumza kule Nyamira baada ya kuzuru vituo mbalimbali vya usajili katika kaunti hiyo, viongozi hao wamewashauri vijana kuwa kadi ya kura ndiyo silaha mwafaka ya kuwatimua mamlakani viongozi waliozembea kazini na kuchagua viongozi wapya.