- 264 viewsDuration: 2:07Wakazi wa kaunti ya Garissa wamehimizwa kufika katika vituo vya usajili wa vitambulisho ama kituo cha Huduma Centre na kuchukua vitambulisho vyao vya kitaifa ili kujisajili kama wapiga kura. Kamishina wa kaunti hiyo Ramadhan Mwabudzo amesema kuna orodha ya watu wengi waliotuma maombi ya vitambulisho na kukosa kuvichukua ilhali viko tayari. Aidha viongozi wa kaunti hiyo waliwarai wenyeji kujiandikisha kwa wingi kama wapiga kura kwenye zoezi linaloendelea.