- 197 viewsDuration: 1:32Wanamazingira kaunti ya Taita Taveta wameanza zoezi la upanzi wa miti katika mbuga ya wanyamapori ya Tsavo kama njia moja ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi. Wanahamazingira hao wamelenga kupanda miti zaidi hasa eneo la Aruba ambako ndovu zaidi ya 300 waliangamia kutokana na makali ya kiangazi miaka ya sabini. Zoezi hilo linaandaliwa kwa ushirikiano na taasisi mbalimbali za serikali ikiwemo shirika la msalaba mwekundu na taasisi ya utafiti wa kisayansi WRTI.