- 6,567 viewsDuration: 4:04Baadhi ya wakazi wa Nguu Tatu na Marimani Kisauni kaunti ya Mombasa wanaishi na wasiwasi wakidai kuna genge la vijana wenye silaha ambao wamekuwa wakivamia mashamba yao na kujenga makazi ya muda. Maafisa wa polisi wamesema wanaendelea na uchunguzi na kutaka waathiriwa kuandikisha taarifa baada ya kupiga ripoti katika kituo cha polisi cha Kiembeni.