- 149 viewsDuration: 1:50Wakazi wa Runyenjes katika kaunti ya Embu wamelalamikia kosefu wa wodi za wanaume katika Hospitali ya Runyenjes. Hali hii inawalazimu wagonjwa kutafuta matibabu katika hospitali za kibinafsi au hospital za umma zilizoko mbali. Wakazi pia wamelalamikia ugumu wa kupata vipimo vya afya katika hospitali hiyo na sasa wanataka serikali ya kaunti ya Embu kuwajibika na kuimarisha utoaji wa huduma za afya hospitalini humo. Hata hivyo Afisa wa huduma za afya katika kaunti ya Embu Jamal Runyenjes amedokeza kuwa ujenzi wa wodi za wanaume umeanza na kwamba huduma za afya zimeimarishwa kwa asilimia 80