Kufuatia wingi wa maembe uliosababishwa na ongezeko la uzalishaji msimu huu, wakulima wanakadiria hasara kubwa kwa kukosa soko la mazao yao.
Hali hiyo imeifanya serikali ya kaunti ya Murang'a kununua maembe katika mpango wake wa kuwalisha watoto shuleni.
Hatua hiyo inalenga kuwalinda wakulima wa maembe kutokana na hasara kubwa ya mavuno mengi. Kaunti hiyo inashirikiana na shirika la Food4Education, kuwalisha zaidi ya watoto 600,000 kila siku. Maembe zaidi ya milioni 1.3 inanunuliwa kutoka kwa wakulima. Aidha wakulima wengi wanakabiliwa na shida ya kuhifadhi maembe.