- 1,240 viewsDuration: 1:32Walimu wa sekondari msingi wanaendelea kuishinikiza serikali kuwapa uhuru wa kujisimamia na kujitenga na shule za msingi. Wakizungumza mjini Voi kaunti ya Taita Taveta waalimu hao wanasema wakati umefika kwa serikali kuangazia malalamishi yao. Aidha wanasema suala la mishahara duni bado halijaangaziwa licha ya wao kupaza sauti katika majukwaa tofauti.