Matumizi ya dawa za kulevya, pamoja na tatizo la ukosefu wa fedha za karo, haswa kwa wanafunzi wa shule za upili na vyuo vikuu, ni miongoni mwa changamoto kubwa zinazowakumba vijana katika kaunti ya Lamu.
Wanafunzi wengi wanaotarajiwa kujiunga na shule za sekondari ya juu na vyuo vikuu katika Kaunti ya Lamu wamesalia nyumbani kutokana na ukosefu wa karo, jambo ambalo linachangia wengi wao kuingia katika dawa za kulevya
Akizungumza kwenye Eid Baraza iliyofanyika Kisiwa cha Amu Gavana Issah Timamy aliwataka wakaazi kuwajibika na kushirikiana ili kukabiliana na wauzaji wa dawa za kulevya mbali na kuwepo kwa juhudi za kuhakikisha watoto wanaendelea na masomo yao