Wanajeshi 8 DRC wahukumiwa kifo kwa kukimbia vita
Mahakama ya kijeshi katika mji wa Goma huko Kivu Kaskazini Mashariki mwa Congo imewahukumu kifo maafisa nane wa jeshi la Congo, FARDC kwa tuhuma za kukimbia vita na kutoheshimu sheria za kijeshi.
Miongoni mwao ni Kanali Shamba mkuu wa kikosi cha makomandoo pamoja na msaidizi wake.
Mwendesha mashtaka amesema makamanda hao walishindwa kuwajibika kwenye uwanja wa mapambano karibu na mji wa Sake wilayani Masisi eneo lililo magharibi mwa mji wa Goma ambako M23 wanaendelea kuchukua udhibiti wa vijiji.
Wakili wa makamanda hao Bwito Jean Richard wa jeshi tiifu kwa serikali amesema mahakama imefanya makosa kutoa adhabu ya kifo kwa wanajeshi hao ambao walikuwa wamejitolea kulipigania taifa.
Hata hivyo amekata rufaa na kuionya Mahakama kuwa makini kwa kuwa hatua za mahakama zinaweza kuwapelekea wanajeshi wengi kutokwenda vitani.
Lakini baadhi ya wachambuzi wamesema hatua hii itawazuia wanajeshi kukimbia mapigano kila mara na kuwaacha waasi kuchukua vijiji.
Katika hukumu hiyo wanajeshi watatu, kapteni mmoja na maluteni wawili waliachiliwa huru na mahakama kwa madai ya kutokuwa na hatia.
Makamanda hao walipewa adhabu ya kifo kwa mujibu wa sheria ya nchi hiyo. Wakati huohuo Mkuu wa mahakama ameziomba pande husika kukata rufaa katika kipindi cha siku tano.
#mahakama #kijeshi #wanajeshi #hukumu #kifo #vita #voa #voaswahili #mahakamayakijeshi
Imeandaliwa na Austere Malivika , Sauti ya Amerika Goma
18 May 2024
- According to the initial plan, the project is projected to cost Ksh4 billion.
18 May 2024
- The appointments followed a series of successful competitive recruitment processes in the past weeks.
17 May 2024
- Kenyans were advised against undertaking outdoor activities for safety reasons.
18 May 2024
- The United Democratic Alliance (UDA) party is conducting its second phase of grassroots election in all the 40 wards within Homa Bay County today (Saturday).
18 May 2024
- A US Supreme Court justice faced calls on Friday to recuse himself from cases involving Donald Trump after an inverted American flag -- a symbol of the former president's false election fraud claims -- was flown outside his home.
18 May 2024
- The head of Canada's Security Intelligence Service warned Canadians against using video app TikTok, saying data gleaned from its users "is available to the government of China," CBC News reported on Friday.
18 May 2024
- Ghana's parliament, which has been adjourned since March following a row between the speaker and the president over an anti-LGBT bill, will reconvene on Friday to discuss approval of ministerial appointees and other "urgent matters".
18 May 2024
- According to the initial plan, the project is projected to cost Ksh4 billion.
18 May 2024
- The appointments followed a series of successful competitive recruitment processes in the past weeks.
18 May 2024
- Spare us wild goose chase in weak impeachment motions
18 May 2024
- Alarm over shortage of newborn jabs as Gavi launches measles drive
18 May 2024
- Puzzle of 2,000 absentee pupils in flood-ravaged Mai Mahiu school
18 May 2024
- Governor Kihika, CEO clash over closure of War Memorial Hospital