- 191 viewsDuration: 1:44Wataalamu wa afya wameeleza kuwa uhamasishaji kuhusu ugonjwa wa saratani unahutaji kupewa kipaumbele, huku wakitaka uchunguzi wa mapema na msaada zaidi kutoka kwa jamii. Mwanzilishi wa shirika linalosaidia wagonjwa wa saratani, Nana Kilemi, amewataka wakenya kufanya uchunguzi wa mara kwa mara, akisema kuwa kugundua ugonjwa mapema kunaweza kuokoa maisha, huku pia akitaka kukomeshwa kwa unyanyapaa na kimya kinachozunguka saratani.