- 271 viewsDuration: 5:04Watu zaidi ya 100 walio na matatizo ya macho wamefanyiwa upasuaji wa bure wa utando wa jicho katika kambi ya matibabu ya macho inayoendelea huko Kirinyaga. Kufikia sasa, watu zaidi ya 1,000 wamefanyiwa uchunguzi kwenye kambi hiyo iliyoandaliwa na Serikali ya Kaunti ya kirinyaga kwa kushirikiana na Huduma za Jamii za Pankaj. Waziri wa afya wa Kirinyaga daktari George Karoki amesema kambi hiyo ya matibabu inatarajiwa kuendelea hadi Jumamosi, Machi 28, na inalenga wakazi 4,000.