Wizara ya afya yasitisha kwa muda leseni ya bidhaa za nikotini

  • | KBC Video
    12 views

    Wizara ya afya imesitisha utoaji wa leseni za bidhaa zote zinazohusiana na nicotine ikiwapa waagizaji, watengenezaji bidhaa, wasambazaji na wauzaji muda wa siku 21 kuwasilisha upya maombi ya kupata leseni mpya katika hatua ambayo waziri wa afya Aden Duale amesema kuwa itapunguza utumiaji wa tumbaku na nicotine humu nchini. Duale aliyasema hayo wakati wa sherehe za maadhimisho ya siku ya tumbaku duniani zilizofanyika mjini Eldoret, kaunti ya Uasin Gishu ambako alisimamia uteketezaji wa zaidi ya tani tano za bidhaa za tumbaku na nicotine zilizonaswa kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Eldoret tangu mwaka 2021.

    Connect with KBC Online; Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKN Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1 Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV Check our website: https://www.kbc.co.ke/

    #kbcchannel1 #news #kbclive