Skip to main content
Skip to main content

Mkasa wa south c: nani wakulaumiwa?

  • | Citizen TV
    1,746 views
    Duration: 3:42
    Maafisa wa upelelezi kutoka vitengo tofauti vya uchunguzi wameanza shughuli ya kukusanya ushahidi kutoka kwa jumba lililoporomoka eneo la South C Nairobi, uchunguzi wa hivi punde ukidhihirisha kwamba uzani wa gorofa tatu zilizoongezwa juu ya jengo hilo, pamoja na ubora wa vifaa vilivyotumika kwa ujenzi ulichochea kuanguka kwa jumba hilo. Majumba yaliyoko karibu na jengo lililoporomoka yanasalia kwenye hatari shughuli ya uokoaji ikikaribia kufikia ghorofa za chini ya jengo hilo