Skip to main content
Skip to main content

Wakazi wa Huruma walalamikia polisi kumpiga risasi Sheryl Anyango, 22 akiwa kibandani

  • | Citizen TV
    15,605 views
    Duration: 3:48
    Ghasia zilizuka katika mtaa wa Huruma eneo la Johnsaga kuanzia jana usiku baada ya polisi kumpiga risasi na kumuua msichana aliyekuwa akiuza samaki kibandani. Msichana huyo Sheryl Anyango alipigwa risasi na kufariki papo hapo, wakati polisi walipokuwa wakilenga mshukiwa wa uhalifu. Ghasia hizo zilizoanza usiku wa kuamkia leo na kuendelea mchana kutwa pia zilisababisha kuchomwa kwa magari matatu na kuharibiwa kwa mali. Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika makafani ya city huku wakaazi wakitaka hatua kuchukuliwa dhidi ya afisa aliyefyatua risasi iliyomuua msichana huyo,