- 371 viewsDuration: 2:50Zoezi la usajili wa makurutu wa polisi ulifanyika Jumatatu, ambapo maelfu ya wakenya walijitokeza katika vituo mbali mbali nchini. Hata hivyo, baadhi yao walilalamikia kile walichosema ni kanuni kali na kuitaka idara ya polisi kulegeza kamba ili kuwaajiri wakenya zaidi. Huku hayo yakijiri, inspekta jenerali wa polisi Douglas Kanja Alisema zoezi hilo limekamilika bila tashwishi yoyote.