Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amewaapisha rasmi wanachama wa tume huru ya uchunguzi wa machafuko yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi mkuu uliofanyika mwezi uliopita nchini humo.tume hiyo imepewa jukumu la kuchunguza kiini cha machafuko hayo pamoja na matamshi ya baadhi ya wanachama wa upinzani yanayodaiwa kuchochea vurugu.na kama anavyoarifu emily chebet, rais suluhu pia ameielekeza tume hiyo kuchunguza mchango wa mashirika yasiyo ya kiserikali, ndani na nje ya tanzania yanayodaiwa kufadhili mapigano