- 391 viewsDuration: 1:25Mbunge wa Malindi Amina Mnyazi ameunga mkono kauli ya kamanda wa polisi Pwani Ali Nuno kuwa wanachama wa magenge mbali mbali ya uhalifu wapigwe risasi akisistiza walinda usalama sharti waruhusiwe kufanya kazi yao. Akizungumza katika chuo cha ufundi Cha Weru, Mnyazi amesema Kwa muda Sasa wakaazi wa eneo hilo wamehangaishwa na magenge hayo yanayowashambuliwa mara kwa mara. Mnyazi anasema wanaopinga amri hiyo ni wale wanaolenga kutumia vijana vibaya Kwa manufaa yao binafsi.