Bodi ya sukari nchini imewahakikishia wakulima wa miwa kuwa serikali inachukua hatua madhubuti kuhakikisha wanapata malipo kwa wakati unaofaa kutoka kwa viwanda vya kusaga sukari. Akizungumza hapa jijni nairobi wakati wa mkutano wa sekta ya sukari barani afrika , afisa mkuu wa bodi hiyo Jude Chesire, amesema mageuzi ya hivi karibuni yamesaidia kurejesha imani ya wakulima, akibainisha kuwa serikali imeweka mikataba ya usambazaji iliyosanifiwa, ambayo sasa ni ya lazima kwa viwanda vyote, ili kuimarisha uwazi na uwajibikaji katika sekta hiyo