- 479 viewsDuration: 1:43Bunduki moja zaidi aina ya AK 47 ikiwa na risasi tatu imesalimishwa na wazee wa jamii ya Orma kwa kamati ya usalama ya kaunti ndogo ya Bangale kaunti ya Tana River. Hatua hii imejiri, kwa kuzingatia makataa ya siku sitini ya kurejeshwa kwa silaha haramu zilizoko mikononi mwa jamii zinazoishi kaunti hiyo. Bunduki hiyo ni ya kumi na mbili ambazo zimerejeshwa pamoja na risasi 28 kufikia sasa na jamii za Orma na Degodia.