Familia zinazoranda mitaani, ambazo hupuuzwa na kudhalilishwa, sasa zinachukua nafasi muhimu katika uhifadhi wa mazingira. Mchango wao katika uhifadhi wa mazingira usiopongezwa na wengi, uliangaziwa katika mtaa wa Dagoreti jijini Nairobi, ambako wadau wa uhisani waliadhimisha siku ya Mazingira na familia za mitaani kutoka Kawangware, yakitambua juhudi zao katika usafi wa mazingira, na pia kwa kuwapa matumaini na usaidizi. Kwa wengi hapa, ujumbe ulikuwa mmmoja, utumikiaji binadamu, ni utumikiaji taifa.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive