- 502 viewsDuration: 2:59Jaji mkuu Martha Koome amewataka mawakili kufanikisha upatikanaji wa haki kwa kutojihusisha na masuala yanayohujumu haki na kuchelewesha kukamilishwa kwa kesi. Akizungumza wakati wa kuwaapisha mawakili 920 katika mahakama ya upeo, Koome pia amepuuzilia mbali shaka iliyoibuliwa kuhusu uapisho wa idadi kubwa zaidi mawakili na kuwataka wanasheria hao kuwajibikia mamlaka yao. Mkurugenzi wa uhariri wa kempuni ya royal media services, Linus Kaikai, alikuwa miongoni mwa mawakili walioapishwa leo