- 1,082 viewsDuration: 3:05Kamati ya bunge la kitaifa kuhusu kawi na Petroli sasa inadai majibu kwa serikali kuhusu shehena ya mafuta iliyozua utata huku sasa ikisema haijaridhishwa na maelezo ya waziri Opiyo Wandayi kuhusiana na sakata hiyo. Kamati hii ya David Gikaria ilifanya ziara katika kampuni ya Kenya Pipeline kutathmini kiwango cha mafuta ambapo imebaini kuwa hakuna uhaba wa petroli. Kamati hii sasa ikitaka leseni za wafanyabiashara wanaoficha mafuta kubatilishwa