Baadhi ya wakurugenzi wa vyama vya ushirika eneo bunge la Sirisia kaunti ya Bungoma, wamewanyooshea kidole cha lawama baadhi ya maafisa wa kampuni za ulinzi kwa kushirikiana na baadhi ya wananchi kuiba kahawa katika vyama vya ushirika.
Mwenyekiti wa chama cha ushirika cha sirisia, martin wataka amedai kuwa tangu kukatizwa kwa kandarasi ya kampuni iliyokuwa na zabuni ya kutoa ulinzi katika kapuni hiyo, hakuna kisa chochote cha wizi wa kahawa ambacho kimeripotiwa.wakulima wameraiwa kukoma kuuza zao hilo katika mataifa jirani msimu huu, wakiahidiwa mapato bora