Kwa nini Trump anakata msaada kwa Afrika Kusini?
Rais wa Marekani Donald Trump Jumapili alidai kuwa serikali ya Afrika Kusini “inataifisha ardhi, na kuwatendea vibaya sana watu wa tabaka fulani.”
“Marekani haitavumilia hilo, tutachukua hatua. Pia nitakata ufadhili wote siku za usoni kwa Afrika Kusini mpaka uchunguzi kamili wa hali hii ukamilike,” Trump alisema.
Hatua ya Trump imekuja mara baada ya Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa kusaini kuwa sheria mswaada wa Utaifishaji Ardhi unaofungua njia kwa serikali kutaifisha ardhi bila yakulipa fidia.
Sheria hiyo ina lengo kupambana na athari za kibaguzi za enzi ya ubaguzi wa rangi Afrika Kusini ambayo ilishuhudia wazungu wachache katika taifa hilo waliokuwa na umiliki mkubwa wa ardhi.
Mamlaka nchini Afrika Kusini zilimjibu Trump Jumatatu nakueleza kuwa sheria hiyo “siyo chombo cha kutaifisha ardhi, lakini ni mchakato wa kisheria uliopitishwa kikatiba ambao unauhakikisha umma unapata ardhi katika usawa na haki kama inavyoongozwa na Katiba.”
Akizungumza wakati wa sherehe za viwanda Jumatatu, Waziri wa Madini wa Afrika Kusini, Gwede Mantashe, alitoa wito wakukabiliana na vitisho vya Trump. Mantashe alisema Trump ana “yaoneya” mataifa madogo kwa sababu “wao ni taifa kubwa.”“Lazima tupinge hilo,” waziri wa madini alisema. - Reuters
#donaldtrump #marekani #afrikakusini #cyrilramaphosa #utaifishajiardhi #sheria #voa #voaswahili #rais
11 Aug 2025
- Youth between the ages of 25 and 34 are the most active online.
11 Aug 2025
- The project aims to ease traffic flow in the city.
11 Aug 2025
- Trump recently spared Kenya from tariff slaps.
11 Aug 2025
- Mexico City's Benito Juarez International Airport suspended operations for several hours Sunday after heavy rains flooded the capital and caused poor visibility, authorities said.
11 Aug 2025
- Countries remained at loggerheads Monday over how to tackle plastic pollution, with only four days left to craft a landmark global treaty on reining in the ever-growing scourge.
11 Aug 2025
- Public Health Principal Secretary Mary Muthoni has warned management of level 2, level 3 and sub county hospitals against charging patients when they seek outpatient medical attention in those facilities.
11 Aug 2025
- Youth between the ages of 25 and 34 are the most active online.
11 Aug 2025
- President Donald Trump pledged on Sunday to evict homeless people from the nation's capital and jail criminals, despite Washington's mayor arguing there is no current spike in crime.
11 Aug 2025
- Israel's military said it killed an Al Jazeera journalist it accused of being a Hamas cell leader in a Gaza airstrike on Sunday, but rights advocates said he had been targeted for his frontline reporting on the Gaza war and Israel's claim lacked…
11 Aug 2025
- The project aims to ease traffic flow in the city.
11 Aug 2025
- They say many have been sitting back and waiting for the state to provide jobs
11 Aug 2025
- Police said one Erick Mutembei Njagi, 53, was shot and killed by four gunmen who were riding on a motorcycle.
11 Aug 2025
- The video widely shared on TikTok claims that the ’23-year-old’ was attacked during a performance.