Skip to main content
Skip to main content

Madereva wanalalamikia kudorora kwa usalama na msongamano barabara za mpaka Kenya-Uganda

  • | Citizen TV
    876 views
    Duration: 3:33
    Madereva wa masafa marefu wanaotumia barabara kuu ya Kisumu kwenda Busia na ile ya Eldoret kuelekea Malaba wanalalamikia kudorora kwa usalama katika barabara hizo, visa vya wizi vikikithiri wanaposubiri katika foleni kuvusha shehena zao mpakani. Wakizungumza kwenye foleni ya magari hayo katika mji wa mpakani wa Busia, madereva hao wameitaka serikali kutafuta suluhu ya kudumu kwa tatizo sugu la msongamano wa malori hayo katika mpaka wa Kenya na Uganda.