- 13,357 viewsDuration: 3:44Familia zaidi ya 500 kutoka mtaa wa Mukuru Kwa Njenga, jijini Nairobi zimeathirika na mafuriko kufuatia mvua kubwa iliyonyesha usiku wa kuamkia leo. Wakazi hao wamelalamikia hasara waliopata baada ya mali yao kujaa maji huku wakieleza hofu ya mkurupuko wa magonjwa. Shughuli za usafiri pia zimetatizika katika barabara kadhaa jijini Nairobi kutokana na mvua hiyo. Wakazi wanahofia hasara zaidi kwani mvua inatarajiwa kuendelea kunyesha.