Muungano wa vyama vya wafanyakazi (COTU) umekosoa matamshi ya kinara wa DCP, Rigathi Gachagua, ambaye alidai kuwa cotu imeshindwa kutetea maslahi ya wafanyakazi na kupendekeza kuundwa kwa muungano mwingine wa wafanyakazi. COTU imesema gachagua hana haki ya kuingilia masuala ya wafanyakazi. Aidha COTU inasema kuwa gachagua hakutetea maslahi yao alipokuwa mamlakani nakuwa hasira zake ni kufuatia nyongeza ya mishahara iliyotangazwa na rais william ruto. COTU imesisitiza kuwa matamshi ya katibu wake francis atwoli kumhusu Rais Ruto yalikuwa maoni yake binafsi.