Skip to main content
Skip to main content

Mwakilishi wa kike kaunti ya Nyamira ataka hatua kali zichukuliwe kwa watu wanaodhulumu watoto

  • | Citizen TV
    98 views
    Duration: 1:10
    Mwakilishi wa kike katika kaunti ya Nyamira Jerusha Momanyi ameomba asasi za usalama kwa ushirikiano na jamii kuchukua hatua kali, dhidi ya washukiwa wa ubakaji wa watoto, kwani visa hivyo vinaongezeka katika kaunti hiyo. Kisa cha punde zaidi kikiwa cha msichana mwenye umri wa miaka 5 kutoka eneo la Gesima aliyebakwa na kisha kuuwawa, huku mwili wake ukipatikana nyumbani kwa jirani yake. Akizungumza katika hafla ya ufadhili wa vyama vya ushirika katika eneo bunge la Mugirango Magharibi, Momanyi amesema visa hivyo vinachangiwa na uraibu wa dawa za kulevya na pombe haramu katika jamii.