Naibu kamishna wa kaunti ndogo ya Nambale, Caroline Onchonka, ameamuru maafisa wa utawala kwa ushirikiano na wazee wa mtaa katika eneo bunge hilo kuhakikisha kuwa wanafunzi wote wa gredi ya kumi ambao hawajajiunga na shule za sekondari ya juu, wamesakwa na kufikishwa shuleni kufikia kesho.
Amesema kuwa juma hili, idara ya utawala kwa ushirikiano na maafisa wa polisi katika eneo bunge hilo watashirikiana kuhakikisha wanafunzi wote wamerejea shuleni. Wazazi wameonywa kuwa watachukuliwa hatua iwapo hawatawapeleka watoto wao shuleni.