Rais Ruto atangaza kuwa serikali itawaongezea marupurupu wawekezaji katika sekta ya uzalishaji

  • | K24 Video
    162 views

    Rais William Ruto ametangaza kuwa serikali itawaongezea marupurupu wawekezaji katika sekta ya uzalishaji wa bidhaa ili kukuza sekta hiyo hadi asilimia 20 ya pato la nchi. Ruto alikuwa akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa kiwanda cha saruji cha kampuni ya cemtech limited katika kaunti ya Pokot Magharibi, ambapo alisema kuwa serikali haitaruhusu kuondolewa kwa ushuru unaotozwa bidhaa zinazoletwa kutoka nje na zinazoweza kutengenezwa nchini. Aidha Ruto alishikilia kuwa serikali haina fedha za kushughulikia matakwa ya madaktari wanaogoma.