- 1,741 viewsDuration: 1:26Rais William Ruto ameamrisha wanafunzi wote kufika shuleni hapo kesho kuendelea na masomo yao akisisitiza kwamba serikali imetoa shilingi bilioni 44 za kufadhili masomo ya bure nchini. Akizungumza katika kaunti ya meru leo katika hafla ya mradi wa nyota, rais ruto aliwataka mchifu na wasaidizi wao kuhakikisha kwamba wanafunzi hao wako madarasani mapema kesho masomo ikiwa wako na karo au la. Wanafunzi wengi wamekwama nyumbani baada ya kukosa karo na sare za shule.