- 721 viewsDuration: 2:47Rais William Ruto hii leo amewahimiza wafanyakazi kuunga mkono azma yake ya muhula wa pili wa urais, akisema kuwa ana tajriba ya kupiga buti ubaguzi na siasa za mgawanyiko. Akizungumza katika Kaunti ya Vihiga, Rais Ruto aliwasuta wapinzani na kusema ataendelea kutekeleza miradi ya maendeleo bila ubaguzi. Viongozi kutoka ukanda wa Magharibi pia walimuunga mkono Rais na kuwataka wakazi wa eneo hilo kujisajili kuwa wapiga kura.