- 293 viewsDuration: 1:29Gavana wa Kaunti ya Bungoma, Kenneth Lusaka, amezindua shughuli ya usambazaji wa ng’ombe wa maziwa katika kaunti hiyo, ili kuongeza kipato cha wakulima wadogo. Mpango huo ni sehemu ya mkakati mpana wa kilimo unaolenga kuboresha lishe ya na kuinua maisha ya wananchi kupitia ufugaji wa ng’ombe wa maziwa, pamoja na miradi ya kuku, samaki, mbuzi na nguruwe. Akizungumza katika eneo la Mukuyuni, Kaunti Ndogo ya Tongaren, Lusaka alisema mpango huo unalenga kuinua viwango vya maisha ya wakulima.