- 182 viewsShule kumi na moja kaunti ya baringo zimefurika kufuatia kuongezeka kwa maji ya maziwa Baringo na Bogoria. Katibu katika wizara ya elimu profesa Julius Bitok ameagiza wanafunzi wanaosomea katika shule hizo wahamishwe mara moja. Hii ni kufuatia hatari inayowakodolea macho wanaposafiri kwenda shuleni na hata kuvamiwa na wanyama wa majini wanapokuwa madarasani.