- 484 viewsDuration: 1:59Uchaguzi wa maafisa wa nyanjani wa chama cha United Democratic Alliance (UDA) unaendelea katika kaunti ya Kwale, wanachama wakiwachagua maafisa 20 katika kila kituo cha kupigia kura kuwakilisha vitengo tofauti. Kufikia sasa uchaguzi huo unaendelea bila matatizo licha ya kuweko kwa kifaa kimoja cha kupigia kura katika kila kituo, huku kukiwa na idadi ya wastan ya wanachama waliojitokeza katika vituo tofauti kushiriki zoezi hilo.