- 287 viewsDuration: 1:22Naibu gavana wa kakamega anaitaka serikali kuu kuanzisha mikakati ya kuwafadhili wanafunzi wasiojiweza kupata elimu ya sekondari ya juu na chuo kikuu. Kiongozi huyo anasema kwamba familia nyingi sasa zinatafuta msaada kutoka kwa viongozi wa kisiasa ili kuwapeleka watoto wao shuleni huku karo na mahitaji mengine ya elimu yakiwalemea wengi. Ametoa wito huu huku wanafunzi wa gredi ya kumi wakitakiwa kuingia shuleni kufikia mwisho wa jumatano.