- 52 viewsUhaba wa madaktari wa meno pamoja na ukosefu wa elimu ya afya ya kinywa katika eneo bunge la Teso Kaskazini kaunti ya Busia umepelekea wengi wa wakazi kupatata matatizo sugu ya meno na kulazimika kuyang'oa. Haya yalibainika kwenye kambi ya matibabu ya bure iliyoandaliwa na madakitari wa meno kwa ushirikiano na chuo cha mafunzo ya kimatibabu (KMTC) cha Kocholia, ambapo mamia ya wakazi wakiwemo wakongwe walijitokeza.Madaktari wamewashauri wakazi nyanjani kufanyiwa ukaguzi wa meno na vinywa angalau mara mbili kwa mwaka ili kuzuia magonjwa sugu.