- 439 viewsDuration: 2:02Wafanyibiashara katika eneo la Onyinjo eneo bunge la Suna magharibi wanakadiria hasara baada ya wezi kuwavamia na kutoroka na bidhaa zao. Wenyeji hao wanalalamikia utovu wa usalama ambao umekita mizizi katika Maeneo hayo. Katika kisa cha hivi punde, wafanyibiashara wengi walipoteza Mali kwani baada ya duka 5 kuvunjwa na bidhaa kuibwa. Wafanyibiashara hao wanaelekeza kidole Cha lawama Kwa maafisa wa polisi ambao wanasema wametelekeza majukumu yao.