- 1,525 viewsDuration: 1:41Baadjhi ya Viongozi wa Embu wamelaani mauaji yaliyosababishwa na polisi wakati wa maandamano huko Ishiara, Mbeere North, ambapo watu watatu sasa wamefariki kutokana na majeraha ya risasi . Gavana wa embu Cecily Mbarire amelaumu polisi kwa kutumia risasi dhidi ya waandamanaji wasio na silaha . Sasa anatoa wito uchunguzi ufanywe haraka ili polisi waliohusika wakamatwe na kushtakiwa. Kamishna wa Kaunti ya Embu, Nalyanya Wanyonyi, pia alikosoa hatua ya polisi, akisisitiza kuwa matumizi ya nguvu kupita kiasi na risasi hayaruhusiwi kisheria. Kulingana naye, maafisa wa mamlaka ya kutathmini utendakazi wa polisi IPOA wanatarajiwa kufika eneo hilo kuanzisha uchunguzi.