- 128 viewsMsemaji wa Serikali ya Tanzania, Greson Msigwa, amesema kuwa chanzo cha maji ni njia nafuu zaidi ya kuzalisha umeme kuliko vyanzo vingine, akibainisha kuwa gharama za uzalishaji wa umeme kwa kutumia maji ni shilingi 30 kwa uniti moja, huku kwa kutumia mitambo ya mafuta gharama zikiwa shilingi 940 kwa uniti moja. Alisisitiza kuwa licha ya kutumia gesi, ambayo imechangia katika uzalishaji wa umeme kwa gharama ya shilingi 170 kwa uniti, maji ni suluhisho la gharama nafuu kwa Watanzania. Msigwa ameeleza kuwa katika mwezi Disemba 2024, kiwango cha juu cha umeme kilifikia megawati 1900, na sasa wastani ni megawati 1880. Amesema bwawa la Mwalimu Nyerere linatoa matumaini makubwa katika kuongeza uzalishaji wa umeme. Aidha, amezungumzia miradi mikubwa ya kuboresha miundombinu ya umeme, ikiwemo mradi wa gridi imara wa zaidi ya shilingi trilioni 4, ambao umekamilika na kupunguza kelele za kukatika kwa umeme. Amebainisha kuwa Serikali inaendelea kujenga miradi ya usafirishaji wa umeme, kama vile njia ya Tanzania-Zambia, ambayo itasaidia kupeleka umeme kwenye nchi jirani. Pia, Msigwa alizungumzia miradi ya njia za kusafirisha umeme kutoka Chalinze hadi Dodoma, na mradi wa kuunganisha gridi ya taifa na nchi za Afrika Mashariki, ambapo Tanzania imefanikiwa kuunganisha na Kenya. Alisema mradi huu utakapokamilika, utawawezesha wateja wapya kupata umeme kutoka kwa gridi ya taifa. Ripoti ya Amri Ramadhani, VOA, Tanzania. #gresonmsigwa #msemaji #serikali #rufiji #mkoawapwani #bwawa #mwalimunyerere #gharama #serikali #voa #voaswahili #tanzania #gharamanafuu
'...uzalishaji wa umeme kwa kutumia maji ni shilingi 30 kwa uniti moja...'
- 30 Apr 2025 - Kenya’s revised foreign policy is designed to address the interests of citizens and reposition Kenya's foreign engagements on the dynamic global landscape, Prime Cabinet Secretary Musalia Mudavadi has said.
- 30 Apr 2025 - President William Ruto’s State Visit to China saw more than 20 trade agreements and memoranda of understanding signed, that aim at improving various sectors of the economy.
- 30 Apr 2025 - The Climate Reality Project, a climate-focused nonprofit founded by former U.S. Vice President Al Gore, is set to host an in-person training event in Nairobi in June.
- 30 Apr 2025 - President William Ruto has praised the increased contributions to the National Social Security Fund (NSSF) as a step toward the country’s financial security.
- 30 Apr 2025 - The MCA is part of the numerous residents that have been the latest targets.
- 30 Apr 2025 - The new fees could prompt an increase in the prices of commodities.
- 30 Apr 2025 - President William Ruto has reaffirmed his commitment to transforming Kenya. He underscored his mission to implement lasting changes for the nation’s development. Speaking in Karen, Nairobi, during the installation of Dr Benard Chitunga as the Chancellor…
- 30 Apr 2025 - Motorists have been urged to cooperate with traffic marshals who will be present on site.
- 30 Apr 2025 - High Court Judge Bahati Mwamuye has declared a protest ban issued by former Nairobi Police Commander Adamson Bungei during the 2024 anti-tax demonstrations illegal and unconstitutional.
- 30 Apr 2025 - Justice Bahati Mwamuye issued the order in a case filed by the Law Society of Kenya (LSK), which had petitioned the court following the killing of Rex Masai during a protest.