- 350 viewsDuration: 8:02Vijana kutoka pembe mbali mbali za nchi wamekongama katika chuo cha MTTI mjini Kajiado kuhudhuria hafla ya ugatuzi inayohusisha vijana ili kujadili nafasi ya vijana kwenye serikali za ugatuzi. Hafla hiyo ambayo imewaleta pamoja zaidi ya Vijana 1,000 kutoka kaunti zote 47 nchini, inalenga kuwapa vijana jukwaa la kuzungumza kuhusu manufaa na changamoto wanazopitia, na pia mchango wa vijana katika uboresha serikali za ugatuzi.